TINDWA AUNGURUMA, ATUA KUCHUKUA FOMU KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KIBAMBA



NA MWANDISHI WETU, KIBAMBA 

Aliyekuwa kiongozi wa Klabu ya  soka ya timu ya Yanga  Beda Tindwa hatimaye amejitosa  kuchuhukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Kibamba lililopo Jijini Dar es Salaam.

Tindwa , amechukua fomu hiyo  katika ofisi za chama cha mapinduzi (CCM) na kusema kwamba ameamua kuingia katika kinyang'anyoro hicho kwa lengo la kuweza kuketa mabadilikl kwa wananchi wa  Jimbo la Kibamba.


Tindwa,amewahi kuwa Mjumbe wa kamati ya utendaji na Mjumbe wa kamati ya mashindano ya Klabu ya Yanga katika kipindi cha mwaka 2013 hadi 2022.

Zoezi la uchukuaji wa fomu katika kuwania nafasi mbali mbali linaendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali katika nafasi za udiwani na ubunge.

Post a Comment

0 Comments