Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa (kulia) pamoja na Kaimu Meneja wa Kampuni ya CRRC International Tang Yun Reng (kushoto) wakisaini mkataba wa ununuzi wa Behewa 1430 za mizigo kati ya Shirika la Reli Tanzania na Kampuni ya CRRC International kutoka nchini China unaogharimu Dola za Kimarekani Milioni 127.2.
NA
ABRAHAM NTAMBARA
SHIRIKA
la Reli Tanzania (TRC) limesaini mkataba wa ununuzi wa behewa 1430 za mizigo ya
Reli ya Kisasa (SGR) ambao unagharimu Dola za Kimarekani milioni 127.2 sawa na zaidi
ya shilingi bilioni 300.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam katika hafla fupi ya utiaji saini mkataba huo Waziri wa Ujenzi
na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa ameiagiza TRC kuhakikisha inasimamia kwa
uzalendo utengenezaji wa behewa hizo ambazo zitatengenezwa na Kampuni ya CRRC Inaternational
ya nchini China.
Waziri
Mbarwa amesema kwamba utengenezaji wa mabehewa hayo unapaswa kukamilika katika
muda uliopangwa kwa mujibu wa mkataba, na kwamba TRC pamoja na timu itakayoenda
nchini China kukagua na kusimamia utengenezaji huo inapaswa kuhakikisha
mabehewa hayo yanakua na ubora unaotakiwa.
“Huu
mradi unatakiwa ukamilike kwa muda uliopangwa naomba nitoe maagizo kwenu Bodi
ya Wakurugenzi wa TRC na timu ya watu mtakaoenda China kuangalia utengenezaji
wa mabehewa haya kuhakikisha mnafanya kazi hiyo kwa uzalendo behewa ziwe na
kiwango cha ubora unaotakiwa, tunataka mradi huu ukamilike kwa haraka ili
ujenzi wa reli unapokamilika mabehewa yawe tayari,” amesema Waziri Mbarawa.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TRC Masanja Kadogosa akizungumzia mkataba
huo, amesema kati ya behewa hizo 1430 zipo za kubeba mafuta, mifugo na magari.
Kadogosa
ameeleza kuwa kwa kiasi kikubwa zitasaidia kukuza biashara nchini na nchi za
jirani ikiwemo Uganda, Rwanda, Burudi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
(DRC).
Hivyo
amesema zitarahisisha usafirishaji na kupunguza gharama za matengenezo ya
barabara pamoja na ajali.
“Behewa
za mifugo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha usafiri wa mifugo kutoka
mikoa mbalimbali ya nchi kwenda kwenye masoko kwa haraka na salama,” amesema
Kadogosa.
Naye
Meneja Mkuu Msaidizi wa Kampuni ya CRRC International Tang Yun Peng
ameihakikishia TRC kufanya kazi hiyo kwa kuzingatia makubaliano yakimkataba
yaliyosainiwa huku akiipongeza Tanzania kwamba endapo mradi wa SGR
utakamilika utafungua milango yakiuchumi kwa nchi zingine za africa Mashariki.
Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania Masanja
Kadogosa (kulia) pamoja na Kaimu Meneja wa Kampuni ya CRRC International
Tang Yun Reng (kushoto) wakionyesha mkataba waliosaini leo wa ununuzi wa Behewa
1430 za mizigo kati ya Shirika la Reli Tanzania na Kampuni ya CRRC
International kutoka nchini China unaogharimu Dola za Kimarekani Milioni 127.2.

Waziri wa ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame mbarawa akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ununuzi wa Behewa 1430 za mizigo kati ya Shirika la Reli Tanzania na Kampuni ya CRRC International kutoka nchini China.

Waziri wa ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame mbarawa akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ununuzi wa Behewa 1430 za mizigo kati ya Shirika la Reli Tanzania na Kampuni ya CRRC International kutoka nchini China.
0 Comments