Mratibu wa Tamasha la ZIFF Prof. Martini Muhando akizungumza jijini Dar es Salaam na Wasanii wa Bongo Movie, wadau na mabalozi wa nchi ambao filamu zao zimebahatika mwaka huu kushiriki.
Matukio mbalimbali katika picha
NA ABRAHAM NTAMBARA
TAMASHA
la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) linatarajiwa kufunguliwa Juni 18 na
kilele chake kuwa Juni 26 mwaka huu.
Hayo
yamebainishwa jijini Dar es Salaam jana na Mratibu wa Tamasha hilo Prof. Martini
Muhando akizungumza na Wasanii wa Bongo Movie, wadau na mabalozi wa nchi
ambao filamu zao zimebahatika mwaka huu
kushiriki.
“Tarehe
18 ndiyo itakuwa siku ya kufungua tamasha, na katika siku hiyo ya tamasha
tutakuwa na filamu moja ambayo itakuwa inaonyeshwa ni filamu ambayo imevunja
rekodi zote hapa Tanzania kwa filamu ambayo ilipendwa sana na sasa hivi
inatembea nchi nzima. Filamu yetu ya kufungua tamasha letu mwaka huu ni ‘Vuta ni kuvute’,” alisema Prof. Muhando na kuongeza,
“Wote
mnaifahamu ni filamu ambayo tunadhani itatuinua kidedea hapa duniani,”.
Hivyo
Prof. Muhando aliwapongeza kina Dkt. Issa Shivji kwa kufanya filamu hiyo ambayo
anaamini itakuwa bora katika Tanzania kwani ni nzuri na yakipekee kufanyika
katika zama hizi.
Aidha
alisema kwamba siku hiyo hiyo ya Juni 18 usiku kutakuwa na watu 15 au zaidi
ambao watakuwa wakitokea Bagamoyo na kuelekea Zanzibar wakiwa katika Jahazi.
“Nia
yetu ni kwamba katika miaka hii ya kuanzia 2015 mpaka 2024, kwa miaka hii 10 ni
miaka ya kusherehekea mchango wa watu weusi katika maendeleo ya Dunia, sasa
Tanzania bado haijafanya chochote katika hilo, lakini sisi tukachukua nafasi
hii ya kusema kwamba tunataka tuonyeshe ulimwengu kwamba sisi Waafrika historia
yetu kwanza tunajivunia historia yetu, lakini vile vile tuko tayari kuchangia
zaidi kwenye maendeleo ya Dunia,” alisema Prof. Muhando na kuongeza,
“Kwahiyo
siku ya tarehe 18 usiku wataondoka watu 15 kuelekea Zanzibar, tutawapokea pale
tarehe 19 asubuhi, wale wageni wetu ni wageni mchanganyiko Watanzania wazawa
pamoja na Wamarekani Weusi ambao walihamia Tanzania baada ya kuona kwamba
wametambua Afrika kama nyumbani kwao. Kwahiyo sisi tutawapokea pale kama watu
huru,”.
Alisema
kwamba mwaka jana kwa mara ya kwanza Serikali ya Marekani ilitambua kwamba hiyo
ni siku muhimu sana kwa watu weuzi au kwa maana ya wenye asili ya Afrika
waishio Marekani kwamba siku hiyo kila mwaka watakuwa wakifanya sherehe.
Prof.
Muhando alisema kwa sababu wanatambua historia kati ya Zanzibar na watu
waliopelekwa utumwani wameamua kwamba watasherehekea siku hiyo visiwani
Zanzibar.
Kwamba
baada ya sherehe hiyo, siku hiyo hiyo ya Juni 19 usiku wataendelea na
uoneshwaji wa filamu nyingine, kwamba Juni 20 wataonesha filamu mchanganyiko
pamoja na warsha kadhaa.
Alibainisha
kuwa tamasha hilo litakuwa na jumla ya filamu 101 ambazo zinatoka nchi 33
kwamba hii inaonesha ni namna gani tamasha hilo ni la kimataifa.
0 Comments