CCM YARIDHISHWA NA UANDIKISHAJI MICHEWENI


Na Mwandishi  Maalum, Pemba 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimeridhishwa na  zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari  la Mpiga  kura katika Wilaya  ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba   kwa mujibu wa sheria na kwa sifa ya kila Mkaazi .

CCM kimeitaja  hatua ya kukosekana malalamiko toka Vyama vyote vya Siasa ni ishara na muendelezo wa  kufanyika chaguzi  huru na za haki Zanzibar.

Hayo yameelezwa Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar,   Idara  ya Itikadi ,Uenezi na Mafunzo  ,Khamisi  Mbeto  Khamis  , aliyesema  kila kitu katika zoezi hilo  kimekwenda kwa murua.

Mbeto alisema wananchi walijitokeza kwa wingi  ili kutumia haki  yao ya msingi na ya kikatiba  ili kujiandikisha na kuwa wapiga kura halali.

Alisema  itakuwa vyema katika majimbo mengine hali ya utulivu ikaendea kama iliofanyika katika majimbo manne ya Wilaya ya Micheweni. 

"CCM  tumeridhishwa jinsi  zoezi lilivyosimamiwa na maafisa wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar. Masheha wametimiza wajibu wao na  kadhalika,".

Post a Comment

0 Comments