MBETO ASEMA CALIFORNIA HAIWEZI KUPATA MAMLAKA KAMILI MAREKANI


Na Mwandishi  Maalum, Dodoma 

CHAMA Cha Mapinduzi kimesema si Republican wala Democratic  chenye uwezo  wa kutaka  Mamlaka kamili huko  Marekani kama ambavyo  ACT  kinavyowadanganya wafuasi  wake Zanzibar .

CCM kimesema sera ya ACT  kutaka mamlaka kamili  Zanzibar ni sawa kuandaa uasi  unaorudisha nyuma maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa miaka sitini.

Matamshi hayo yametamkwa na Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC Zanzibar , Idara  ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis,  akijibu mapigo  ya Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo ,Othman Masoud Othman. 

Othman  ndiye Makamo wa Kwanza  wa Rais  SMZ , alikuwa akihutubia mkutano  wa hadhara huko Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja aliyesema  mwaka 2025 ni wa kuipatia  Zanzibar Mamlaka kamili.

Mbeto akijibu  hoja hiyo, alimtaka  Othman  kuacha kuwadanganya wazanzibari kuwasimulia  hadithi  kongwe  na kuwapa  ahadi amabazo  ACT  Wazalendo  hakiwezi kuzitekeleza.

Akitoa mfano ,Mbeto   alisema  Marekani  yenye  Muungano wa Mataifa 52 , hakuna hata nchi  moja (jimbo)kati  ya hizo ,yenye  uwezo wa kutaka ipate mamlaka yake  kamili ndani  ya Taifa la  Marekani 

"Othman acha kudanganya na kutoa ahadi hewa . Wewe ni msomi wa sheria.  Act hakina ubavu wa  kuvunja Muungano wa Tanzania  . Hata Florida, Ohio  au  California  inayoweza kupata mamlaka kamili  Marekani " Alisema Mbeto. 

Aidha  Mwenezi  huyo aliwataka viongozi  wa ACT  kuacha propaganda  hasi ambazo  zimekuwa zikiwafanya wapuuzwe   na wananchi toka mwaka 1995 kwa kunadi  sera hiyo inayowakosesha ushindi  kila uchaguzi Mkuu .

"Baada ya miaka sitini na moja ya Muungano ni wazimu mtu  kufikiria kuvunja  Muungano . Ujasiri ni kuzungumzia changamoto zinazoukabili Muungamo na kuzitatua  si kupata  mamkala kamili " Alieleza Mbeto 

Alisema si taifa la Tanganyika wala Zanzibar  ambalo kwa sasa linaweza kuibuka na kutaka   mamlaka  kamaili ndani ya  Tanzania,  kwa kufanya hivyo ni sawa na kuunda  uasi au  kufanya Mapinduzi 

"Kila wakati  watu wazima kudai mambo  yasiowezekana ni kuonyesha wasivyo na maarifa.Acheni kupiga  mayowe twendeni kwenye  masanduku ya kura Oktoba  mwaka huu mkakione cha mtemakuni " Alisisitiza Mbeto  

Pia Mwenezi  huyo alisema wakati kuna watanzania waliowekeza  rasilimali ,mitaji na  miradi  yenye thamani  kila yoande wa Muungano, hawatounga mkono sera hiyo isio na  manufaa kwa maisha  yao.

pia katibu mwenezi amewashukuru wananchi wa wilaya ya wete kwa kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha kwa amani na utulivu na kutimiza haki yao ya kikatiba na kisheria kwa kuzingatia kwamba ni haki ya kujiandikisha kwa mujibu wa sheria namba 4 ya mwaka 2018 ibara ya 15 ambayo ndio inasimamia suala la uandikishaji.

Wananchi wa wilaya ya wete yenye majimbo matano 5 ambao wote wameweza kupata fursa ya kujiandikisha kwa wingi na kutimiza matakwa ya sheria ya tume ya uchaguzi na kupata haki yao na fursa ya kujiandikisha ili wapate fursa ya kuja kuwachagua viongozi wao wakati ukifika wa uchaguzi mkuu October.

Post a Comment

0 Comments