MBETO: ASIYEONA MAENDELEO YALIOLETWA NA RAIS DKT. SAMIA AKAPIME MACHO


Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

Chama cha Mapinduzi  (CCM) kimesema mtanzania  yeyote  ambaye hataona kazi kubwa ya kimaendeleo iliofanywa na Serikali  ya Rais  Dk  Samia  Suluhu  Hassan ,haraka  aende kituo chochote  cha Afya akapime uoni wa macho yake .

Pia chama hicho  kimejigamba  kuwa maendeleo ya haraka  yaliopatikana katika awamu ya sita, yamezistusha nchi nyingi jirani na kuupongeza utawala  wa Rais Samia .

Matamshi hayo yametamkwa na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar  ,idara ya Itikadi, Uenezi  na Mafunzo , Khamis  Mbeto Khamis ,aliyesema  Rais Dk Samia  amefanya maajabu  katika uongozi wake kwa kusimamia sera za maendeleo. 

Mbeto alisema kazi ya usimamiaji na utekelezaji wa miradi  mbalimbali ya kihuduma na kimaendeleo imetekelezwa kwa ufanisi na serikali   , hivyo haihitaji kuona kwa tochi,badala yake yaliofanyika  yanaonekana.

Alisema   Rais Dk Samia  ni kati ya marais ambao wametimiza  vyema majukumu na wajibu wao mbele ya wananchi kwa kuendeleza  na kuanzisha miradi  ya kupigiwa mfano  ambayo  imeacha alama zisizofutika.

'Tanzania  ya leo itabaki kuwa mfano mbele  ya Mataifa  mengine Barani  Afrika. Serikali  ya awamu ya sita imefanya maajabu makubwa sana. Mikoa yote imepata mabadiliko  kiuchumi huku wananchi wakiishi maisha bora"Alisema Mbeto

 
Akitoa mfano ,Katibu huyo Mwenezi  , aliitaja sekta ya afya chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ,  Tanzania imetambulika na Asasi za Kimataifa na kupokea Tuzo Maalum ya Kimataifa ya Global Goalkeeper 
Award kutoka Taasisi ya Gates Foundation.


Aidha Tuzo hiyo inaashiria kutambua mchango na  jitihada zilizofanywa kwenye sekta ya afya na mafanikio ya Serikali ya 
Tanzania katika kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya umri wa miaka mitano. 

Alisema Tuzo hiyo ambayo hutolewa kwa viongozi waliowezesha nchi zao kuharakisha maendeleo kuelekea 
kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu (Sustainable Development Goals –SDG’s) imekabidhiwa kwa Rais 
Dkt. Samia na Dkt. Anita Zaidi, Rais wa Kitengo cha Usawa wa Jinsia kutoka Taasisi ya Gates.

“Kati ya mwaka 2020 hadi 2024 uwekezaji uliofanywa 
na Serikali kwenye sekta ya afya imewezesha Tanzania 
kuongeza vituo vya kutolea huduma za afya vinavyotoa huduma za dharura za mama na mtoto kutoka 340 
hadi 523". Alieleza Mbeto 


Pia Wataalamu wabobezi wa kiafya wa masuala ya mama na 
mtoto wameongezeka kutoka 69 hadi 338, na kuongeza 
mashine za Ultrasound na Somograph kutoka 345 hadi 
970.

 Mbeto  alisema mwaka 2020 Hadi 2024 serikali  ya Rais  Dk Samia iliongeongeza Vituo vya  Afya Maalum kwa Mama na Mtoto .

Post a Comment

0 Comments