Mbeto amshangaa OMO kuzungumzia zbar kugawana madaraka akiwa Uingereza


Na Ahmada John, Zanzibar

Chama Cha Mapinduzi kimesema ACT Wazalendo   hakiwezi kuafiki ukweli  wowote kati yake na CCM zaidi ya chama hichi  kila wakati kudhani demokrasia ya kweli ni CCM kuondoka madarakani .

Pia kimekanusha  hakuna waraka wowote au makubaliano yatakayofanyika kati ya CCM na ACT  yanayotaja kugawana madaraka.

Matamshi hayo yametamkwa  na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar  Idara  ya Itikaadi  ,Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis,  aliyesema kitendo  cha Mwenyekiti  wa ACT Wazalendo  Othman Masoud Othman,  kuwalalamikia  Doaspora huko Uingereza ni matumizi mabaya ya wakati. 

Mbeto  alisema makubaliano ya kimsingi kati ya CCM na ACT   ni kuendeleza  Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar yanayotajwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984.

Alisema si kweli kama kulikuwa na mpango wa kugawana madaraka  kama inavyodaiwa na   Othman au  wakati  wa Hayati Maalim Seif  sharif Hamad alipokuwa Makamo wa Kwanza wa Rais SMZ   . 

"Hata ukisoma Katiba  ya Zanzibar ya Mwaka 1984 hakuna kipengele  chochote au Ibara ya katiba inayotaka kuwepo na  kugawana madaraka SMZ " Alisema Mbeto .

Aidha, alisema hata walipokutana kati ya aliyekuwa Rais wa Zanzibar Awamu ya saba,  Rais Mstaafu Dk Amani Karume na aliyekuwa kiongozi  wa upinzani  ,Hayati Maalim  Seif  Sharif  Hamad, hakukuwa na kabrasha la makubaliano yoyote ya aina hiyo.

"Makubaliano ya msingi ni baada ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar  kukiondoa  kipengele cha katiba ya Zanzibar  kilichosema anayeshinda achukue vyote na kutajwa kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar "Alieleza 

Mbeto  alisema mjadala wa  kugawana madaraka Zanzibar, haukufikia tamati toka katika mazungumzo ya kupata suluhu yaliofanyika Bagamoyo Mkoa wa Pwani  ambapo Wajumbe wa CUF walisusia mazungumzo hayo.

"Mazungumzo yaliogusia kutaka kugawana  madaraka  ni  kati  ya CCM na CUF si na ACT  Wazalendo. Hata hivyo  mazungumzo hayo yalikufa baada ya viongozi  wa CUF kuikimbia meza ya upatanishi "Alisema Mbeto 

Katibu huyo Mwenezi  alisema viongozi wa  CUF  walipokimbia mazungumzo  hayo ,baadae Dk Karume na Maalim Seif  wakakutana faragha ikulu  Novemba 9 mwaka 2009 na kufikia muafaka usio na maandishi .

"OMO hayajui yaliofikiwa kwakuwa wakati  huo hakuwa  mwanachama wa CUF wala ACT. Anahadithiwa na kupotoshwa na wanaompa taarifa hizo . Aonyeshe kabrasha la makubaliano  yaliofikiwa kati  yake na Rais Dk Mwinyi au na Maalim seif "Alisisitiza Mbeto.

Post a Comment

0 Comments