MBETO: RAIS DKT. SAMIA KIELELEZO CHA KIONGOZI MWANADEMOKRASIA AFRIKA



 Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi  kimeitaja hotuba iliotolewa na Rais   Dk Samia Suluhu  Hassan wakati   akivunja Bunge la 12 ,  imeleta matumaini mapya ,  kurudisha  ari  na kukua kwa haiba ya ustawi wa  Kisiasa, kiuchumi ,kijamii na kidemokrasia nchini.

Vile vile,CCM  kimekiri Rais Dk Samia  amefanya  juhudi kubwa,akitumia akili,  nguvu za  kulitumikia Taifa  toka  alipochukua kijiti kufuatia kifo cha mtangulizi wake Hayati Dk  John  Magufuli.

Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar, Idara ya Itikadi  , Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis, ameiita hotuba hiyo  ni kabambe iliothibisha uwezo alionao na utendaji wenye  ufanisi wa Serikali  yake .

Mbeto aliseema kupanda kwa takwimu za  ukuaji uchumi, pato ghafi la Taifa  ,ukusanyaji mapato ya ndani  na  deni la Taifa ikiwemo   shilingi ya Tanzania kukua  huku mfumuko wa bei ukishuka  kuwa  hayo ni mafanikio ya kujivunia  .

Alisema mauzo ya bidhaa  za uzalishaji w ndani nje ya nchi, Akiba ya Fedha za kigeni iliopo ,Akiba ya  Hifadhi  ya chakula , juhudi za kupambana n rushwa na dawa za kulevya , yamempa  Rais na serikali  yake heshima ya kipekee .

"Kupitishwa kwa idadi ya Miswada Bungeni na kuwa sheria. Kuwepo uhuru wa habari, Vyama vya Siasa kufanya shughuli zake na msikumo wa  kupatikana katiba mpya  siku zijazo ni umadhubutu wa Serikali yake"  Aliswma Mbeto 

Kuhusu uhuru wa mawazo ,  utoaji wa maoni, kusajili vyombo vipya vya habari ili  kufanyakazi zao,ni fursa inayohimiza kasi ya uwajibikaji,kutanuka kwa wigo  wa demokrasia  na utendaji unaoleta tija na ufanisi. 
Aidha , Mbeto aliyataja masuala  yote hayo,  si aghalab kuyakuta katika baadhi ya nchi duniani hususan Barani  Afrika ,lakini  chini ya uongozi wa Rais Dk  Samia , yote yamewezekana .

"Hotuba  ya Rais Dk  Samia amekunjua mbawa za uongozi wake katika  azma ya kuliongoza Taifa. Amejipambanua na kuonyesha umakini  alionao katika  kutumikia Taifa na  wananchi wake" Alieleza Mbeto 

Katibu huyo Mwenezi  aliongeza kusema hotuba hiyo ya Mkuu huyo wa Nchi , imeelezea kwa  kina na  juhudi  mbalimbali za kimaendeleo  zizochukuliwa  ikiwemo mikopo , kukua kwa deni la Taifa kutokana kupanda kwa  thamani  dola .

"Ilikuwa ni  hotuba  yenye msisimko yenye kila sababu  ya kuungwa mkono na watanzania wote . Unapoyatazama maendeleo yaliostawi nchini  kila Mtanzania anakiri  awamu ya sita  imetimiza wajibu wake" Alieleza.

Hata hivyo Mbeto aliitaja fomula ya RNne chini ya utawala wa  Rais Dk Samia ,imeifanya serikali  yake kuwa ni uongozi  kidemokrasia na kiongozi anayefuata utawala wa sheria  na kuenzi  haki za binadamu .

Post a Comment

0 Comments