LONGIDO DC YAJIPANGA KWA MAPOKEZI YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, AWALI NA DARASA KWANZA




NA ABRAHAM  NTAMBARA

Halmashauri ya Wilaya ya Longido imejipanga kuhakikisha Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, Awali na Darasa la Kwanza walioasililiwa kwa muhuMa wa Masomo wa Mwaka 2026 wanaanza masomo Shule zinapofunguliwa Januari 13, 2025.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido Mhe. Thomas Ngobei akizungumza baada ya ziara ya siku mbili ya ameanza ziara ya siku mbili ya kukagua maandalizi ya upokeaji wa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, Awali na Darasa la Kwanza kwa muhula wa masomo wa mwaka 2026 hususan kwa shule mpya wilayani humo iliyoanza Disemba 30 na kukamili leo Disemba 31, 2025.

Amesema kwa maandalizi yaliyofanyika na yanayoendelea kufanyika ni matumaini yake kuwa ifikapo Januari 13, 2026 wanafunzi wote wanaostahili kuanza masomu muhula wa mwaka 2026 wataanza masomo yao bila vikwazo vyovyote.

Hivyo ametumia fursa hiyo kuwahimiza wazazi kuhakikisha watoto wao wanaripoti shule zitakapofunguliwa bila kukosa kinyume na hapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa watakaokaidi.

“Tumetembelea shule, tumepita kuhakiki maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi kwa mwaka 2026. Longido tumejipanga na tupotayari kwa mapokezi ya Wanafunzi,” amesema Mhe. Ngobei.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, Afya na Maji Mhe. Obedy Mollel amesema kuwa baada ya kutembelea shule hizo wameridhika na maandalizi kwani wamehakikishiwa na wakuu wa shule kuwa wamejipanga kwa mapokezi ya wanafunzi.

“Shule hizi tumejiridhisha kwamba wamejipanga kwa mapokezi ya wanafunzi. Walimu wakuu wametuhakikishia wanafunzi wote watapokelewa na kuendelea na masomo yao,” amesema Mhe. Mollel.

Aidha amewapongeza wananchi kwa kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kushirikiana na viongozi wa Kata na Vijiji kutatua baadhi ya changamoto kwa kuchangia baadhi ya mahitaji ikiwemo viti, meza na vitanda kwa ajili ya kuweka mazingira rafiki kwa wanafunzi shule zitakapofunguliwa.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido Mhe. Peter Lekaneti ametumia fursa hiyo kuwahimiza wananchi kuanza kutatua changamoto zinapotokea na Serikali itakuja kuongeza nguvu ili kumaliza changamoto hizo.

Katika siku ya kwanza ya ziara hiyo Mhe. Ngobei alijionea maandalizi katika Shule Shikizi ya Laalaroi na Shule ya Sekondari Noondoto zilizopo Kata ya Noondoto. Aidha, alitembelea Shule ya Sekondari Mundarara na Shule ya Msingi Lesing’ita, zote zilizopo Kata ya Mundarara.

Kadhalika kwa siku ya pili ya ziara Mhe. Ngobei alitembelea Shule ya Sekondari Kimokouwa, Shule ya Sekondari Kamwanga, Shule ya Msingi Kamwanga, Shule ya Sekondari Sinya, Shule ya Msingi Sinya, Shule ya Sekondari ya Wasichana Longido Samia pamoja na Shule ya Msingi Oltepes.

Katika ziara hiyo, Mhe. Ngobei aliambatana na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Peter Lekaneti; Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji, Mhe. Obedy Mollel; Kaimu Afisa Elimu Sekondari, Bw. Mgonza Salehe; pamoja na Kaimu Afisa Elimu Msingi, Bw. Mustafa Kaisi.


Kwa mujibu wa ratiba ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, shule za Awali, Msingi na Sekondari zinatarajiwa kufunguliwa rasmi Januari 13, 2026.

Post a Comment

0 Comments