Na Victor Masangu, Pwani
Serikali ya awamu ya sita katika kupambana na changamoto ya ukosefu wa ajira imeamua kuja na mpango kabambe wa kuanzisha shindano linalojulikana kwa jina la Vijana uchumi Challenge lenye lengo la kuwakutanisha vijana mbali mbali ili waweze kutoa kutoa mawazo yenye kuleta tija katika kuisaidia serikali katika nyanja mbali mbali ikiwemo uchumi na maendeleo.
Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Ofisi ya Rais maendeleo ya vijana Dkt. Kedmon Mapana wakati wa halfa ya uzinduzi rasmi wa kambi maalumu kwa ajili ya usahili wa vijana wapatao 100 bora ambao wamepata fursa ya kuchaguliwa kati ya vijana elfu 7852 walioshiriki hapo awali kutoka mikoa mbali mbali ipatayo 27 ya Tanzania bara na visiwani.
Pia amebainisha kwamba ana imani vijana hao 100 ambao wamechaguliwa na kuweka kambi wataweza kuleta matokeo chanya na kwamba serikali itaendelea kushirikiana nao bega kwa bega na kuchukua mawazo yao ambayo watakwenda kuyafanyia kazi na kuyaendeleza katika maeneo mbali mbali.
"Sisi kama serikali tumeona ni muhimu sana kuwashirikisha vijana wetu wa Tanzania ambao ndio Taifa letu la kesho katika shindano hili ili waweze na wao kuchangia mawazo yao mbali mbali ambayo yataweza kuketa tija zaidi katika kuisaidia serikali katika nyanja mbali mbali za kiuchumi na mambo mengine ya kimaendeleo na mimi nashukuiru sana vijana hao 100 kwa kujitokeza kwa wingi,"amesema Naibu Katibu huyo.
Kadhalika amesema kwamba baada ya kambi hiyo ya vijana watachaguliwa kutoka 100 hadi kufikia vijana 10 ambao watakwenda katika shindano la fainali litakalofanyika mwezi ujao tarehe 6 na kwamba mshindi wa kwamba atajinyakulia shilingi milioni 50, mshindi wa pili milioni 30 na mshindi wa tatu milioni 20 na wengine waliobaki watapewa kifuta jasho.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Kitaifa ya shindano hilo la vijana Uchumi Challenge Joseph Malekele amesema kwamba washirki hao wataweka kambi kwa kipindi cha muda wa siku nne katika katika shule ya Uongozi Mwalimu Julias Nyerere iliyopo Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani ambapo pia watapatiwa mafunzo kutoka kwa jopo la majaji mbali mbali.
Mwenyekiti huyo amesema kwamba lengo kubwa la kuandaa shindano hilo ni kuweza kupata mawazo bunifu kutoka kwa vijana ambayo yanaweza kutekelezeka na kuchangia kwa kiasi kikubwa masuala mazima ya kukuza uchumi pamoja na kuweka misingi endelevu katika maendeleo katika sekta mbali mbali za kilimo, usafirishaji, biashara na mambo mengineyo.
Nao baadhi wa vijana hao ambao wamepata fursa ya kuingia katika kambi hiyo akiwemo Raiani Amour na Adrian Thomas wamebainisha kwamba wana imani mawazo na ubunifu wao utaweza kwenda kuleta matokeo chanyaa katika kuwasaidia vijana hasa ambao wamekuwa na changamoto katika ukosefu wa ajira.
Aidha wameipongeza kwa dhati serikali ya awamu ya sita kwa kushirikiana na Wizara ya vijana kwa kuweza kuona umuhimu mkubwa wa kuwakutanisha vijana kutoka maeneo mbali mbali kwa ajili ya kutoa mawazo yao mbali mbali ili kuweza kuisaidia serikali katika mambo mbali mbali.
Kilele cha Shindano hilo la Vijana Challenge kwa mwaka wa 2026 linatarajiwa kufanyika tarehe 6 ya mwezi ujao Jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan,


0 Comments