NA MWANDISHI WETU
Serikali imeendelea kuhimiza
uendelezaji na matumizi ya nishati jadidifu kama sehemu ya mkakati wa kuongeza
upatikanaji wa nishati ya uhakika na endelevu kwa maendeleo ya kijamii na
kiuchumi nchini.
Akizungumza katika Kongamano la
Siku ya Nishati (Energy Day) linaloendelea katika Ukumbi wa Mwandoro, Viwanja
vya Mwalimu Julius Nyerere – Sabasaba, jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi
anayeshughulikia Nishati Jadidifu, Mha. Imani Mruma, alisema nishati jadidifu
ina mchango mkubwa katika kupanua upatikanaji wa nishati na kuharakisha
maendeleo ya sekta hiyo.
Mha. Mruma alieleza kuwa Serikali
inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhamasisha matumizi ya vyanzo vya
nishati jadidifu kupitia ubunifu, matumizi ya teknolojia na utekelezaji wa
mikakati inayolenga kuongeza uwekezaji na upatikanaji wa nishati safi na
endelevu.
Aliongeza kuwa juhudi hizo
zinalenga kuhakikisha nishati jadidifu inachangia kikamilifu katika kufikia
malengo ya maendeleo ya Taifa na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi.

0 Comments