"ZEGE" LA MCHAKATO WA MARIDHIANO HALILALI- ASEMA MBETO



Na Mwandishi  Wetu,Zanzibar

Chama Cha Mapinduzi kimesema kinaridhishwa na juhudi mahususi zilizochukuliwa hatua kwa hatua , na Rais Dk Samia Suluhu Hassan  kuelekea ,hatimaye kupata  Muafaka, suluhu na  Maridhhano ya Kitaifa .

CCM pia kimeutaja uamuzi  wa  Rais kuanza kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii, Wanataaluma, Viongozi wa Dini Wanasiasa, Uundaji wa Tume za Haki Jinai na Tume ya Uchunguzi ni  hatua endelevu .

Hayo yamebainishwa na Katibu  wa Kamati Maalum  ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi ,Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto  Khamis,  aliyepoulizwa kuhusu ukimya na hatua za maendeleo ya mchakato wa kufikia maridhiano ya Kitaifa na mahali zilipofikia .

Mbeto akijibu swali hilo,alisema kinachoendelea si ukimya juu ya ufumbuzi wa suala hilo, badala yake masuala  yote kwa umuhimu wake ,yanaendelea kufanyiwa kazi  huku yakifuata taratibu sahihi  ,mazungumzo na uthabit wake.

Alisema Rais Dk Samia amekuwa akifuatilia na kuzingatia kila hatua , kwa ukaribu unaostahili  pamoja na kuhakikisha makundi yote katika jamii,  yanapata nafasi ya  kushiriki ,kutoa maoni na kusikilizwa.

"Mchakato wa kufikia Maridhiano wenye lengo la  kuponya yaliotokea ni kama zege .Zege likishachanganywa na kuwekwa kokoto, mchanga na saruji  halilali.Rais bado yuko kazini usiku na mchana"Alisema Mbeto. 

Aidha , Mwenezi  huyo aliwaeleza Waandishi wa Habari waliofika Ofisini kwake kuulizia mchakato  huo, alijibu akisema hatua zote zinazochukuliwa na Rais, zina baraka na kukiridhisha Chama Cha Mapinduzi .

"CCM na Serikali  zake haziwezi kupuuzia jambo nyeti linalobeba maslahi na maisha ya jamii na kuliacha likibaki njia panda.Kazi inaendelea kwa kasi yenye kuridhisha na mchakato  wake unaelekea kukamilika" Alieleza

Katibu huyo Mwenezi alisema hata hatua ya Rais kukutana na viongozi wa Vyama Vya Siasa, kamati ya Baraza la  Maaskofu (TEC) ,Viongozi Wastaafu na Wanasheria ni katika juhudi za kufikia uponyaji unaokusudiwa.

Hata hivyo Mbeto  alisifu mkakati  wa Rais  Dk Samia wa  kuanzisha Tamasha la Kizimkazi ambalo ndani yake ,alisema limekuwa likijumuisha  miradi dhidi  umasikini ,kutumia fursa za elimu na uhamishaji wa miradi ya kijamii. 

Alisema Tamasha hilo linajitanua  kiutendaji kwa kufikia malengo yake na  kuwepo ushiriki  mkubwa wa jamii jambo huku likikuza haiba na taaswira ya kitaifa ,kikanda na kimataifa.

"Ubunifu na  kuwepo  Tamasha  hili umeilenga jamii .Tamasha limejikita katika kupambana na  maadui Ujinga,Umasikini na Maradhi. Limekuwa kioo na alama muhimu katika jamili "Alifafanua Mbeto.

Post a Comment

0 Comments