BINTI SHUPAVU WATOA ELIMU YA HEDHI SALAMA SHULE YA MSINGI MSASANI ‘A’

Mwenyekiti wa Binti Shupavu Hadija Seif akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Msasani A iliyopo wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam.


Bondia wa Kimataifa wa Tanzania Selemani Kidunda akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Msasani A iliyopo wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam.


Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Msasani wilayani Kinondoni Mkoani Dar es Salaam akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Msasani A wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam (aliyevaa nguo ya njano).



Habari katika picha

NA ABRAHAM NTAMBARA

TAASISI ya Binti Shupavu imetoa elimu ya hedhi salama kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Msasani ‘A’ iliyopo wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo ulioambatana na utoaji wa msaada wa taulo za kike kwa wanafunzi hao, Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Hadija Seif ambaye pia ni mwandishi wa habari wa Michuzi Media amesema kuwa lengo lao ni kuona mabinti wanakuwa shupavu na kupinga vishawishi ambavyo vitawafanya kutotimiza ndoto zao.

“Kwanini Binti Shupavu, lengo ni kuona mabinti wanakuwa shupavu na kusimama wenyewe na kupinga vishawishi, tunaangalia wasichana ambao wanapata vishawishi na kukatiza ndoto zao,” amesema Hadija na kuongeza kwamba,

“Tupo tayari kukemea hivyo vishawishi na kuwaambia mviepuke ili mfikie ndoto zenu,”.

Amewataka wanafunzi hao kuwa huru kumweleza mzazi/mlezi wa kiume wanapokuwa katika kipindi cha hedhi ili waweze kupata huduma stahiki ikiwemo kununuliwa taulo za kike.

“Na unatakiw akujenga urafiki na ndugu zako wa damu, kama vile baba, mama, mjomba, bibi, shangazi na sio watu wengine wakiwemo bodaboda ambao watakuingiza katika vishawishi hatarishi,” amesema Hadija.

Kwa upande wake Mwanamasumbwi wa Tanzania Selemani Kidunda akizungumza kwa niaba ya akina baba, amesema kwamba Binti Shupavu ni yule ambaye anajiamini na mwenye uwezo wa kuepuka vishawishi hatarishi.

Aidha amewataka watoto wa kike kutambua kwamba hedhi sio ugonjwa na kwamba wanapokuwa katika kipindi cha hedhi wasiogope kuwaambiwa wazazi wao yaani baba na mama.

“Baba ni kama mama usiogope kumwambia, ukipata tatizo mshirikishe ili akusaidie,” amesema Kidunda.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii Kata ya Msasani wilayani Kinondoni Mkoani Dar es Salaam, Kichiki Njovu amewataka watoto wakike wanapokuwa na tatitizo wasiwaeleze watu wa barabarani na badala yake wawaambie wazazi au waalimu kwa msaada zaidi.

“Usimwombe msaada mtu yeyote barabarani mfano bodadoda kwani hata kupa msaada bure. Mwisho wake utapata ujauzito na kushindwa kutimiza ndoto zako kwani hedhi ni chanzo cha kupata ujauzito,” amesema na kuongeza kuwa,

“Kwahiyo sasa hivi ukikutana na mwanaume utapata ujauzito, ukipata ujauzito nani atakutunza, unakuta wazazi wengine ni wakali wanakufukuza,”.

Hivyo amewataka watoto hao wakike wajitunze kwamba wasikimbilie kupata mimba za utotoni.

 

 

Post a Comment

0 Comments