Rais wa Taasisi ya Wahandisi Tanzania (IET) Mhandisi Dkt. Gemma Modu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
NA MWANDISHI WETU
TAASISI ya Wahandisi Tanzania (IET) inatarajia kufanya Kongamano
la 32 la Kitaifa (National Conference) Novemba 30 hadi Desemba 2 Mwaka huu
katika Ukumbi wa Kimataifa Arusha (AICC), jijini Arusha.
Hayo yamebainishwa leo Novemba 23, 2023 na Rais wa IET
Mhandisi Dkt. Gemma Modu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es
Salaam.
Mhandisi Dkt. Modu amesema Kongamano hilo wanaliandaa kwa
kushirikiana na Bodi ya Usaili wa Wahandisi (ERB) na Chama cha Wahandisi
Washauri Tanzania (ACET).
“Tunatazamia Wahandisi, mafundi wanafunzi na wadau wengine
kutoka mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi watashiriki Kongamano hili muhimu
na kuna baadhi ambao watashiriki kwa njia ya mtandao. Tunakadiria kuwa na
washiriki zaidi ya elfu moja (1000),” amesema Mhandisi Dkt. Modu.
Kwamba katika Kongamano hilo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa.
Amesema dhima ya mkutano huo ni “Innovative Solutions in
Engineering for Sustainable Development” ambapo kwa tafsiri ni “Suluhisho za
Ubunifu katika Uhandisi kwa Maendeleo Endelevu).
Mhandisi Dkt. Modu ameeleza kuwa dhima hiyo na kwa kuzingatia
kwamba leo Dunia ipo kwenye zama za utandawazi wa Karne ya 21.
“Na tunaishi kwenye uchumi na jamii, zinazoendeshwa kwa
nguvu ya Teknolojia ambayo maendeleo yake ni makubwa na ya Kasi na
yanayochochewa zaidi na Mapinduzi ya kidigitali na unaandamana na Ubunifu wa
kisayansi na matumizi yake ni ya lazima ili kuleta tija katika uzalishaji wa bidhaa,
Utoaji huduma na uendeshaji wa Mifumo,” ameongeza Mhandisi Dkt. Modu na
kueeleza,
“Kwa kuzingatia hayo, tunapaswa kufahamu kuwa, utekelezaji
wa mikakati mbalimbali ya Maendeleo unahitaji sio tu Kukuza ujuzi na maarifa katika
Uhandisi bali pia Kukuza kiwango na uwezo wa Ubunifu wa kisayansi na Teknolojia
na ujuzi nyingine muhimu za Karne ya 21 zikiwemo nidhamu, umakini, ufanisi, uwezo,
juhudi, weledi, uwajibikaji na kadhalika,” ameeleza Mhandisi Dkt. Modu.
Mhandisi Dkt. Modu ameeleza kuwa lengo ni ili kuweza
kuendana na kukidhi matakwa ya Maendeleo ya Teknolojia na kuweza kusaidia Nchi
kutatua changamoto katika Sekta mbalimbali za kiuchumi, pia kutoa suluhusho la
matatizo katika jamii.
Ametumia fursa hiyo kuwakaribisha Wahandisi na wadau wote wa
Sekta mbalimbali za uchumi nchini kushiriki kwenye Kongamano hilo muhimu.
Amewakumbusha Wahandisi na mafundi ambao bado hawajajiunga
na Taasisi ya Wahandisi wajounge.
Kwa upande wake Mjumbe wa Baraza la Utendaji wa IET Mhandisi
Pendo Haule akizungumza kuhusu ushiriki wa Wahandisi wazawa kwenye Miradi ya
Serikali, amesema wamekuwa wakishiriki.
Kwamba Serikali imekuwa ikiwashirikisha kama Kampuni moja moja ama kwa Wahandisi kuungana na
kuchukua tenda.
Mfano wa miradi ambayo Wahandisi wazawa wameshirikishwa ni
katika ujenzi wa Mradi wa miundombinu ya Mawasiliano.
Hivyo ameomba na kuhimiza makampuni ya wazawa kujitokeza
kuchukua Miradi pindi inapotangazwa ili kuonesha ujuzi na utaalam wao.




0 Comments