KOKA AREJESHA RASMI FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KIBAHA MJINI



Na Victor Masangu, Kibaha

Mbunge mteule  wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) amerejesha leo fomu rasmi  kwa ajili ya kugombea nafasi ya ubunge Jimbo hilo na kuahidi kushirikiana bega kwa bega na madiwani wote ambao wameteuliwa katika kuleta mabadilko chanya ya kimaendeleo katika nyanja mbali mbali.

Akizungumza  na wanachama wa CCM pamoja na wananchi pamoja na viongozi mbali mbali ambao wamejitokeza kwa wingi kwa ajili ya kumsindikiza katika zoezi hilo la urudishaji wa fomu amebainisha kwamba endapo atapata fursa ya kuchaguliwa tena katika nafasi hiyo ataendeleza  kusikiliza kero na chanagmoto za wananchi na kuweza kuzitafutia ufumbuzi.

Aidha Koka amesema kwamba kwa sasa wanachama wote wa CCM wanapaswa kumpa ushirikiano wa kutosha kwa lengo la kuweza vunja makundi na kushikamana kwa pamoja lengo ikiwa ni kuweza kumpa kura nyingi za kishindo kwa nafasi ya  Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan, wabunge pamoja na nafasi ya udiwani.

"Nawashukuru sana wana ccm wote  wa Jimbo la Kibaha mjini kwa kuweza kuniamini na kunipa kura nyingi katika mchakato wa kura za maoni na leo hii nimeweza kupata fursa y kuweza kurejesha fomu  kwa ajili ya kuweza kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Kbaha mjini naa kwamba taratibu zote zimekwenda vizuri na fomu zote ambazo zinastahili tayari nimeshazirejesha,"amebaisha Koka.

Aidha amebainisha kwamba kwa sasa hivi kitu kikubwa ni kuhakikisha wanawekaa misingi imara ambayo itaweza kuleta maabadiliko makubwa katika suala zima la kuweza kupata kura nyingi za kishindo katika kuelekea  uchaguzi mkuu ambao unatarajiwa kufanyika Octoba mwaka huu wa 2025.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Nyamka amesema kwa sasa zoezi la mchakato wa kura za maoni tayari umeshamlizika hivyo wagombea walioshindwa pamoja na wanachama wote kuvunja makundi yote  na kuwa kitu kimoja lengo kubwa ni kuwa na  nguvu ya pamoja ambayo itasaidia kuweza kushinda  kwa kishindo katika uchaguzi mkuu.
                                         
                                                                                        

Post a Comment

0 Comments