DR.NICAS ACHAGULIWA NAFASI YA UMEYA HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA



NA MWANDISHI WETU ,KIBAHA 

Diwani mteule wa Kata ya Tumbi  Dkt. Nicas Mawazo amechaguliwa kuwa Meya mteule wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha baada ya kupata kura 15 kati ya kura halali zipatazo  19 ambazo zimepigwa na madiwani  wateule wa chama cha mapinduzi (CCM)  huku Aziza Mruma akichaguliwa kuwa katika nafasi ya Naibu meya kwa kupata kura 10 .

Akitangaza matokeo hayo ya uchaguzi wa ndani wa chama Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Issack Mawazo amebainisha kwamba zoezi zima uchaguzi huo umemalizika  salama na kwamba viongozi  hao wateule wanatarajiwa kuapisha Disemba 4 mwaka huu  

Katibu huyo amefafanua kuwa zoezi hilo la uchaguzi limekwenda vizuri na kwamba  wagombea wote wameridhishwa na matokeo hayo na kuwahimiza viongozi hao kuvunja makundi na badala yake wawatumikie wananchi.


Kwa upande wake Meya mteule kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM ) Dr,Nicas Mawazo  amesema kwamba uchaguzi huo umeendeshwa kwa haki na uhuru na kwamba matarajio yake makubwa ni kushirikiana na madiwani wenzake katika kuwaletea chachu ya maendeleo ikiwa pamoja na kuwapambania wananchi walio wanyonge.

 Naye Naibu Meya mteule  waa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Aziza Mruma amesema kuwa lengo lake kubwa ni kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo.

Viongozi hao waliochaguliwa katika nafasi za Meya na Naibu Meya   Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha wanatarajiwa kuapishwa rasmi  Disemba 4 mwaka huu.

Post a Comment

0 Comments