AFISA MAENDELEO KATA YA MUNDARARA NA MATALE APATIWA PIKIPIKI KUTEKELEZA SHUGHULI ZA JAMII




NA MWANDISHI WETU

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bi. Grace Mghase, leo Januari 20, 2026, amemkabidhi Pikipiki aina ya Boxer Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Mundarara na Matale, Bw. Zephania Nyalyoto.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bi. Mghase alisema kuwa pikipiki hiyo itarahisisha utekelezaji wa shughuli za Maendeleo ya Jamii, hususan ufuatiliaji wa marejesho ya mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri na usajili wa vikundi vya huduma ndogo za fedha.

“Leo namkabidhi pikipiki Bw. Zephania Nyalyoto, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Mundarara na Matale, ili imrahisishie katika shughuli za Maendeleo ya Jamii, hususan kufuatilia urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10 na usajili wa vikundi vya huduma ndogo za fedha,” amesema Bi. Mghase.

 


Post a Comment

0 Comments