WIZARA YA NISHATI YASISITIZA USHIRIKIANO KUIMARISHA MAENDELEO YA SEKTA YA NISHATI

NA MWANDISHI WETU

Wizara ya Nishati imesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, taasisi zilizo chini ya wizara, sekta binafsi na wadau mbalimbali katika kuharakisha maendeleo ya sekta ya nishati na kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

Akizungumza katika Kongamano la Siku ya Nishati (Energy Day) linaloendelea katika Ukumbi wa Mwandoro, Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere – Sabasaba, jijini Dar es Salaam, Mhandisi Mkuu wa Nishati, Bw. Christopher Nyondo, alisema Wizara ya Nishati inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa kushirikiana na taasisi zilizo chini yake katika kusimamia maendeleo ya sekta hiyo.

Bw. Nyondo alieleza kuwa wizara inaendelea kuratibu shughuli za sekta ya nishati, kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na kuimarisha upatikanaji wa nishati kwa lengo la kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuboresha ustawi wa wananchi.

Aliongeza kuwa ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, taasisi za nishati, sekta binafsi na wadau wengine ni msingi muhimu wa kufanikisha malengo ya maendeleo ya sekta hiyo na kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Kongamano hilo limewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kujadili fursa za uwekezaji, ubunifu na maendeleo yanayoendelea katika sekta hiyo nchini.


Post a Comment

0 Comments