NA ABRAHAM NTAMBARA
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam Godwin
Gondwe amewataka wakuu wa vikosi vya Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama
Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuwachukulia hatua kali madereva
wasiofuata sheria.
Gondwe ametoa kauli hiyo leo katika viwanja vya Mnazi
Mmoja jijini Dar es Salaam wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama
barabarani kwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam.
“Lengo ni ili kunusuru vifo, majeraha na ulemavu kwa
wananchi,” amesema Gondwe.
Hata hivyo amewataka wananchi wasiwe mashabiki wa mwendo kasi
wanapokuwa kwenye vyombo vya moto na badala yake watoe taarifa kuhusu madereva
wanaoendesha kwa kasi na kutofuata sheria za barabarani.
Akizungumzia maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani
kwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam amelipongeza Jeshi la Polisi Kikosi cha
Usalama Barabarani kwa kupeleka askari trafiki kutoa elimu ya usalama
barabarani mashuleni, na maeneo mbalimbali ikiwemo katika vijiwe vya bodaboda.
Hata hivyo Gondwe amesema ili kufanikisha mapambano dhidi
ya ajali za barabarani ni lazima kila mtu kutimiza wajibu wake.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Kanda Maalumu
ya Dar es Salam ZTO Abduli Isango amesema katika kipindi cha maadhimisho hayo Jehi
la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani kilitoa elimu ya usalama barabarani
katika shule 14 za jijini Dar es Salaam.
“Tulitoa pia elimu kwa madareva bodaboda na madereva bodaboda zaidi ya
2,000 wamepata elimu hiyo. Madeva wa magari pia zaidi ya 2,000 wamepata elimu. Vile
vile tumetoa elimu kwa askari wa usalama barabarani,” amesema ZTO Isango.
Naye Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ajali kutoka Hospitali ya Muhimbili Kitengo
cha Mifupa (MOI) Dkt. Joseph Mwanga amesema kuwa wagonjwa wanaowapokea kwa
kiasi kukibwa zaidi ya asilimia 50 ni waajali za pikipiki.
“Wanakuwa wameumia sana kuanzia kwenye mfumo wa ubongo, miguu na
kifuani. Wiki hii pekee tumepokea majeruhi 42 na zaidi ya 30 wanahitaji
upasuaji wa mifupa,” amesema Dkt. Mwanga.
Dkt. Mwanga amesema mgonjwa akishakuwa katika hali hiyo anakuwa dhaifu
na hawezi kurudi katika hali yake ya kawaida na kuweza kufanya shuguli zake za
uzalishaji hali ambayo inaathiri familia kwani anakuwa mzigo wa kuhitaji msaada
wa kuhudumiwa.
HABARI KATIKA PICHA
0 Comments