Mganga
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Rashid Mfaume
NA ABRAHAM NTAMBARA
MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt.
Rashid Mfaume amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuwa mstari wa mbele
katika mapambano ya Uviko-19 kwa kuhamasisha wananchi kuchanja.
Shukurani hizo alizitoa akizungumza jijini
Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Qaswida za ujumbe wa Uviko-19
(Corona 2022).
“Kubwa ni kuendele kuwashukuru viongozi wa
dini na nitoe rai kwa viongozi wengine pia wa dini mbalimbali wa madhehebu
mbalimbali kuiga hiki kitendo kizuri ambacho kinafanyika,” alisema Dkt. Mfaume.
“Matokeo ya kuwaunganisha viongozi wa dini
katika hizi hamasa za kupambana na Uviko-19 tumeona mfano hata kwenye uchanjaji
Mkoa wa Dar es Salaam idadi ya watu ambao wananchanja kwa siku imeongezeka
sana. Kwa sasa tunachanja hadi watu 6000 kwa siku,” aliongeza.
Akizungumzia kuhusu mashindano hayo ya
Qaswida alisema kuwa Januari 21 mwaka huu walikutana na viongozi wa dini na
kuwaomba waangalie ni namna gani watatoa mchango wao katika kuhakikisha
wanawahamasisha wananchi kuchanja.
Hivyo aliwashukuru Bakwata kupitia Jumuiya
yake ya Vijana kwa kuja na ubunifu huo kwani licha tu ya vijana hao kushiriki
mashindano hayo bali yataweza kutoa elimu kwa wananchi na hatimaye kuwasukuma
kupata chanjo ya Uviko-19.
“Leo hii tukio ambalo liko mbele yetu tuna
uzinduzi wa uimbaji wa Qaswida wenye jumbe mbalimbali za kupambana na Uviko-19,
na sisi hapa kama Serikali kwa kweli tuendelee kuwashukuru sana viongozi wetu
wa Dini.
“Tulikutana nao Januari 21 mwaka huu,
tukawaomba watusaidie kwa namna wanavyojua kuanzisha aina ya ubunifu ambao
wanaujua wanaoweza wakaufanya ili watusaidie kufikisha jumbe mbalimbali kwa
waumini lakini kupitia kwa waumini naamini kwamba jamii nzima itakuwa imepata
ujumbe,” alisema.
Aidha Dkt. Mfaume aliwashukuru wadau wa
maedeleo wakiwemo Shirika la MDH kwa kuunga mkono jitihada
hizo.
“Na kwa keli nichukue nafasi hii
kuwashukuru wenzetu wa MDH hawakusita kuwasapoti wenzetu viongozi wa dini baada
ya kuona kwamba mara nyingi viongozi wa dini wanapopata fursa wanapowezeshwa
wamekuwa ni wa msaada mkubwa,” alisema.
Aidha kwa vijana waliojitokeza kushiriki
mashindano hiyo Dkt. Mfaume aliwataka waendelee kutiwa moyo kwa sababu kwa wao
ni mashindano lakini kama Serikali inaangalia thamani ya wao kushiriki na
ujumbe ambao watautoa kwenye mapambano dhidi ya Uviko-19.
“Kwa hiyo tumewasihi kati ya wale ambao
bahati mbaya hawataweza kupata fursa ya kushinda katika hatua nyingine wasikate
tamaa, tunawategemea sana wakatufikishie jumbe hizo, wananchi waendelee
kuchukua tahadhari ya matumizi ya barakoa, matumizi ya Sinitizer na kuchanja,”
alisema.
Kwa upande wake Msimamizi wa Miradi yote ya
MDH kwa upande wa Mkoa wa Dar es Salaam Ally Kaduma alimshukuru Mgang Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam na Bakwata kupitia Sheikh Pembe kwa kuwaunganisha katika
kupambana na Uviko-19.
”Mnajua kwamba sasa hivi tuna kwenda kwenye
jamii na mkumbuke na Jamii inalinwa na Dini inalinwa na Imani na Imani
inasimamiwa na Dini. Na Dini moja wapo ambayo inasimamia Imani yetu Dini ya
Kiislam na Bakwata ni Baraza ambalo linasimamia Imani yetu,”.
Hivyo alisema kama MDH wanashirika kwa sababu
wanakwenda kupambana na virusi vya Corona, kwamba Bakwata wamejitolea kuwa
mstari wa mbele katika mapambano hivyo na wao wapo kwa ajili ya kuwaunga mkono.
0 Comments