Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa Benki ya Equity Tanzania Rojas Mdoe akizungumza katika hafla fupi ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Karibu Memba’ jijini Dar es Salaam.
NA
ABRAHAM NTAMBARA
BENKI
ya Equity Tanzania imezindua kampeni ya ‘karibu memba’ yenye lengo la kuwashukuru
wateja kwa kufanya nao huduma kwa miaka 10 toka ianze kutoa huduma nchini.
Akizungumza
katika hafla fupi ya uzinduzi wa kampeni hiyo leo Juni 1, 2022 jijini Dar es
Salaam Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa Benki hiyo Rojas Mdoe amesema wateja ni
sehemu ya familia yao kwamba ndiyo maana wanawaita memba.
“Tumewahudumia
kwa muda wote na kuwa vinara katika utoaji wa huduma kidigitali kama Dunia ya
sasa inavyotaka, pia benki ipo mstari wa mbele kutoa huduma mbalimbali za
kifedha ikiwa ni pamoja na, utunzaji fedha, Akaunti za watoto, vikundi, mikopo
mbalimbali kama ya wakulima (kilimo biashara/Agribusiness), wastaafu,
wafanyabiashara kubwa na ndogo ndogo, waajiriwa, watumishi wa umma na kadhalika,”
amesema Mdoe na kuongeza kwamba,
“Akaunti
zetu zote hazina makato ya kila mwezi na gharama za wakati wa kutoa au kutuma
ni nafuu ukilinganisha na mabenki mengine,”.
Mdoe
ameeleza kwamba ndani ya miaka 10, Benki ya Equity imeweza kutoa ajiri kwa
Watanzania zaidi ya 430 na kubadilisha maisha ya Watanzania zaidi ya 500
kiuchumi na kijamii.
“Hivi
karibuni tuliweza kuzindua mradi na taasisi mbalimbali kwa ajili ya mikopo ya
wakulima tukiunga mkono Serikali katika kuhakikisha tunaipa nguvu sekta hii ya
msingi katika ukuaji wa uchumi wa nchi yetu. Tuna makubaliano na taasisi
mbalimbali kama Agricom na Yara ili kuhakikisha kuwa wakulima wanapata pembejeo
kirahisi na kwa gharama nafuu,” ameongeza Mdoe.
Amebainisha
kwa Benki hiyo imejikita katika kutatua changamoto za wananchi na itaendelea
kutoa elimu na fursa mbalimbali zinazotolewa na benki kwa memba wa Tanzania na
Dunia kwa ujumla.
Hivyo
ametoa wito kwa wananchi wengine kujiunga na benki hiyo na kufurahia huduma zao
mbalimbali kama za mikopo nafuu ili kuwafikia wafanyabiashara wadogo wadogo,
wakulima wadogo na wakubwa, wakina mama na jamii nzima katika kuendelea
kujikwamua kiuchumi.
Amesema
kuwa Benki hiyo ni benki pekee yenye huduma nafuu na za kisasa/kidigitali
kwamba hivi karibuni wamezindua kampeni yao mpya ya benki kidigitali inayoitwa
ISHI KISASA-PESA MZIGO ikiwa na lengo la kusisitiza matumizi ya huduma za
kibenki za kidigitali zinazoweza kumfanya mteja kupata huduma popote alipo bila
hata kufika benki.
0 Comments