COMORO MWENDA AUTAKA UBUNGE JIMBO LA KAWE, achukua fomu kuomba ridhaa ya chama


NA MWANDISHI WETU

MBOBEZI wa Kazi katika Utumishi wa Umma Kimataifa, Comoro Mwenda (kushoto), amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kumpitisha kugombea Ubunge Jimbo la Kawe. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 29, 2025 mkoani Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Mwenda amesema anauzoefu mkubwa katika kufanya kazi na mashirika makubwa ya kimataifa.

Hivyo amesema kuwa hajachukua fomu kama fasheni bali anania thabiti ya kuwatumikia wananchi endapo atapatiwa ridhaa ya chama chake cha CCM.

Mwenda, amekabidhiwa fomu na Katibu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Amos Richard.

Post a Comment

0 Comments